
Ruben Van Parsie akiifungia Arsenal goli pekee katika mchezo wao dhidi ya Queens Park Rangers. Hilo lilikuwa goli la 50 kwa Van Parsie kwa klabu pamoja na timu ya Taifa kwa mwaka huu wa 2011

Van Parsie akishangilia goli lake dhidi ya QPR. Mchezo huo ulimalizika kwa Arsenal kushinda kwa goli 1 - 0

Stephen Ireland akiisawazishia goli timu yake ya Aston Villa dhidi ya Chelsea. Mchezo huo uliochezwa Stamford Bridge ulimalizika kwa Aston Villa kuifunga timu ya Chelsea goli 3 - 1

Petrov wa Aston Villa akiifungia timu yake goli la pili dhidi ya Chelsea

Darren Bent akikamilisha goli la tatu na la ushindi dhidi ya Chelsea.

Grant Hanley akishangilia goli lake na la ushindi wakati timu yake ya Blackburn Rovers ilipoibuka na ushindi dhidi ya Manchester utd katika uwanja wa Old Trafford. Blackburn walishinda 3 - 2

Alex Ferguson baada ya mchezo kati ya Manchester united na Blackburn, ambapo Manchester walifungwa goli 3 - 2


Juu Rafael Van de Vaart wa Tottenham akiifungia timu yake goli la kuongoza dhidi ya Swansea na chini yake wachezaji wenzake wakimpongeza.

Scot Sinclair wa Swansea (kati) akipongezwa na wachezaji wenzake baada ya kufunga goli la kusawazisha dhidi ya Tottenham. Mchezo huo ulimaliza kwa sare ya 1 - 1
Orlando Sa wa Fulham akishangilia goli lake aliloifungia timu yake na meneja wake Martin Jol. Mchezo huo ulimalizika kwa sare ya 1 - 1

Jackson wa Norwich akishangilia goli lake la kusawazisha dhidi ya Fulham katika dakika za majeruhi. Mchezo huo ulimaliza kwa sare ya goli 1 - 1

Steven Gerrard wa Liverpool akiifungia timu yake goli la tatu dhidi ya Newcastle. Mchezo huo ulimaliza kwa Liverpool kushinda goli 3 - 1

Steven Gerrard akishangilia goli lake dhidi ya Newcastle pamoja na meneja wake Ken Daglish






























.jpg)

