Msaada wako unahitajika

Mchango wako unahitajika kuchangia kununua hili Temple na kulifanya kuwa shule ya kiislamu hapo Leicester mjini (Leicester Town Centre). Jengo lina sehemu kubwa kabisa (Hall) ya kufanya msikiti. Inshaallah tukifanikiwa itakuwa ndio msikiti wa kwanza kuwa Town Centre hapa Leicester. Toa kwa ajili ya Allah, chochote utakachotoa ni sawa na sadakat jariya kwani malipo yake yataendelea hata kama utakuwa umetangulia mbele ya haki. Jazakallah Khayr Kwa maelezo zaidi tafadhali wasiliana nasi: madrasatulnoor.01@gmail.com

Saturday, 14 April 2012

Liverpool yatinga fainali ya kombe la FA Uingereza

Head boy: Carroll flicked home the winner from a free-kick in the 87th minute
Andy Carrol akishangilia goli lake na la ushindi kwa timu yake ya Liverpool

Bao la Andy Caroll katika dakika za lala salama katika mechi ya nusu fainali ya Kombe la FA dhidi ya Everton katika uwanja wa Wembley, limeipatia Liverpool tiketi ya kucheza fainali ya Kombe la FA nchini Uingereza.

Nikica Jelavic alikuwa wa kwanza kuipatia timu yake ya Everton bao la kuongeza baada ya kuitumia nafasi nzuri iliyojitokeza wakati walinzi wa Liverpool Jamie Carragher na Daniel Agger walipokosa mawasiliano na kujichanganya katika kuokoa hatari iliyokuwa golini mwao.

Time it right: Luis Suarez pulled his side back level shortly after the hour mark
Luis Suarez akiipatia Liverpool bao la kusawazisha

Makosa ya mlinzi wa Everton Sylvain Distin kutoa pasi kwa kipa wake Tim Howard ambapo mpira huo ulikuwa mdogo ndipo mshabuliaji wa Liverpool Luis Suarez aliitumia nafasi hiyo kwa kuuwahi mpira huo na kuutumbukiza mpira wavuni.

Na ndipo mnamo dakika ya 87 mchezaji ghali wa kingereza Andy Carroll, aiweza kuamsha mayowe ya wapenzi wa Liverpool waliokuwa katika uwanja huo wa Wembley kwa kuunganisha kwa kichwa mpira wa adhabu uliopigwa na Craig Bellamy.

Liverpool sasa imejiweka katika nafasi nzuri ya kuweka mkobani Kombe la FA, baada ya tayari kuweka kibindoni Kombe la Carling.

No comments:

Post a Comment